Breaking News

PICHA: Uzinduzi wa Wasafi Tv kwenye StarTimes

Msanii wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz ametangaza rasmi kuingia ubia na king’amuzi cha Startimes ambacho kitarusha matangazo ya Wasafi Tv.

Siku ya jana Diamond Kupitia ukurasa wake wa Instagram alitangaza kuwa atakuwa na mkutano na waandishi wa habari katika hoteli ya Slipway siku ya leo saa tano asubuhi.

Diamond amezindua rasmi Wasafi Tv ndani ya Startimes Tanzania Bara na visiwani ambayo itakuwa inaruka Live Kupitia chaneli namba 444 katika king’amuzi hiko.

Wasafi Tv tayari inapatikana katika king’ Cha Azam na sasa unaweza kuipata kupitia king’amuzi cha Startimes.
Hizi ni baadhi ya picha za matukio yaliyojiri ukumbini hapo:

No comments